
1.
Mungu ni Mungu
tu, hata kama huamini kuwa Mungu yupo yeye atabaki kuwa Mungu.
2. Kuna siku yale waliyokufundisha/kuonya/kuelekeza
wazazi/walezi wako utayashuhudia kwa macho yako mwenyewe.
3. Unahitaji kujifahamu vizuri wewe mwenyewe,
uhodari wako, udhaifu wako na uwezo wako wa katika Nyanja mbalimbali. Itakusaidia
sana.
4. Ukiweza kuokoa muda umepiga hatua kubwa sana
maishani; mimi huona ukiweza kuokoa muda ni sawa na kushinda nusu ya vita
unazotakiwa kupambana hapa duniani.
5. Kuna watu kwenye maisha watakufanyia wema ambao
kamwe huwezi kuwalipa.
6. Kila mtu ana pande nne, uzuri, ubaya, ujasiri na
udhaifu; Hivyo ni juu yako kuchagua
upande gani utautazama.
7. Jitahidi kwa uwezo wako wote kuwa na amani na
kila mtu/kuishi vizuri na kila mtu.
8. Mahusiano yanahitaji muda, pesa, akili,na nguvu
zako; kama haupo tayari usiingie.
9. Unaweza kuwa mtu muhimu sana kwa mtu lakini sio
muda wote; hivyo usijisahau soma alama za nyakati.
10. Mtu ambae ni mwema kwako lakini ni katili(anafanya
mabaya) kwa wengine; hata wewe hakufai.
11. Tafuta taarifa/maarifa sahihi, muda mwingine
unaweza kuhangaika sana na tatizo ambalo suluhisho lake linafahamika.
12. Matumizi ya pesa yafanywe na akili yako na sio moyo wako.
13. Kuna nyakati mbaya zitakupata ili kukuokoa na
nyakati mbaya zaidi zilizopo mbele yako; hivyo usilaumu kila jambo lina sababu.
14. Wema/uzuri wako unaweza kukuingiza matatizoni
pia; hivyo ukifanya jambo usitegemee mrejesho chanya pekee hataka umefanya
mema.
15. Muda mwingine ukicheka unaweza kueleweka vibaya hata
kama hukucheka kwa ubaya; hivyo tabasamu zaidi kuliko kucheka.
16. Jitahidi kuwaelewa watu kwa matendo yao kuliko
kuwafahamu kwa maneno yao.
17. Jitahidi katika mipango yako usimtegemee
mwanadamu yeyote.
18. Mahangaiko yote ya duniani ukifuatilia mwisho wa
siku ni kutafuta furaha; hivyo fanya kile unachokipenda.
19. Unaweza kutazama maisha ya mtu na ukajifunza
somo kubwa ambalo vitabu havijapata kuandika, wahamasishaji hawajawahi kuongea
na waigizaji hawajawahi kuigiza; *penda kujifunza kwa mifano inayoonekana.
20.Jifunze angalau kitu kimoja kila siku, kifupi
usichoke kujifunza. Na zaidi ya yote jifunze kupitia makosa yako ili uzidi
kukua siku hadi siku.